Without Any Reason Quotes

Quotes tagged as "without-any-reason" Showing 1-1 of 1
Enock Maregesi
“Akili yangu itakaponipeleka kwa mgonjwa hospitalini halafu sekunde hiyohiyo jicho langu likacheza au kiungo changu chochote cha mwili kikauma na kuacha ghafla ‘bila’ sababu yoyote, najua kile ninachokifikiria kuhusu mgonjwa huyo ama kitatokea au hakitatokea. Nikifikiria amepona, halafu ghafla kichwa kikaniuma na kuacha, kitakuwa kinyume chake. Yaani, hatapona. Nikifikiria amekufa, halafu ghafla kichwa au kiungo kingine chochote kikaniuma na kuacha, kitakuwa kinyume chake pia. Yaani, hatakufa. Hivyo, nikifikiria amepona, nikifikiria amekufa, na kichwa kikaniuma na kuacha, sekunde hiyohiyo natakiwa kumwombea mgonjwa huyo. Kama ni kupona, apone kama Mungu alivyokusudia; na kama ni kufa, afe kama Mungu alivyokusudia. Si kama Shetani alivyokusudia.”
Enock Maregesi