Kitu Quotes

Quotes tagged as "kitu" Showing 1-8 of 8
Enock Maregesi
“Usisubiri Mungu afanye kitu ambacho Mungu anasubiri ufanye.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Ukiona kitu ambacho hukupaswa kuona, au ukisikia kitu ambacho hukupaswa kusikia, fumba macho kwa kuyakodoa! Ulichokiona au kukisikia usikiseme leo na hata milele. Jifanye hukuona kitu, hukusikia kitu. Ukifumbua macho kwa kuyakodoa utapata matatizo, makubwa.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Kama umefanya au umesema kitu kibaya na ukasema ukweli mbele ya mtu au ya watu, omba msamaha kupata tena kibali cha umma.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Ukitaka kuwa na mashabiki fanya kitu ambacho si cha kawaida katika maisha yako, kila siku.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Ukitaka kumsahau mtu au kitu usimchukie au usikichukie kwa sababu kuchukia kuna nguvu sawa na kupenda.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Tafuta kitu cha kufanya katika maisha yako unachokiamini zaidi kuliko pesa, kutoa sauti kwa ajili ya watu wasioweza kusikika kwa mfano, na ukishakipata kuwa kiongozi na mkarimu kwa wengine. Kutoa sauti kwa ajili ya watu wasioweza kusikika inaweza kuwa ndiyo nafasi yako uliyopangiwa na Mungu uitumie kwa manufaa ya wengine, si kwa manufaa yako, nafasi za wengine zitatumika kwa manufaa yako. Kuna vitu vingi ambavyo mtu anaweza kufanya; chagua kimoja kinacholeta maana zaidi katika maisha yako na ukifanye hicho, kwa nguvu zako zote.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Pesa ina thamani pale unapokuwa nayo, si pale unapokuwa huna, hivyo iweke mahali unapoweza kuiona: katika nyumba, katika shamba au katika elimu. Badala ya kumpa mtu pesa ili ajenge nyumba, mpe nyumba. Badala ya kumpa mtu pesa ili afanye biashara, mpe biashara. Halafu, mpe elimu afanye maamuzi ya biashara yake. Pesa ina laana na Mungu pekee ndiye anayeweza kuiondoa laana hiyo. Ni rahisi kwa tajiri kupata baraka ya pesa kwa sababu ana pesa na ana uwezo mkubwa wa kusaidia maskini. Ni vigumu kwa maskini kupata baraka ya pesa kwa sababu hana au ana uwezo mdogo wa kusaidia maskini. Mungu anaweza kuondoa laana ya pesa kupitia hisani kwa maskini, kitu ambacho aghalabu hufanywa na matajiri wenye uwezo mkubwa. Heri kutoa kitu au huduma au elimu kwa maskini kuliko pesa.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Unapotenda wema kwa mtu au kitu huwezi kujua ni kitu gani kizuri au kibaya kitatokea kwako au kwa mtu mwingine baadaye kupitia wema ulioutenda.”
Enock Maregesi